Mayasa Mariwata
Ilikuwaje? Taarifa ikufikie kuwa, staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael `Lulu’ aliibua minong’ono kwenye msiba wa mwanamuziki Ramadhan Masanja `Banza Stone’ baada ya kutaka kumsalimia kwa kumshika mkono mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma
Chanzo chetu kilichoshuhudia tukio hilo
lililojiri hivi karibuni kilisema kuwa Lulu aliingia nyumbani kwa wazazi
wa Banza, Sinza-Lion, Dar ili kuwasalimu wafiwa lakini baada ya kumuona
Mama Salma Kikwete alijisogeza jirani kwa lengo la kutaka kumsabahi
lakini walinzi wake walimzuia kwa kuwa ni kinyume na utaratibu.
Baada ya kubwagiwa ‘ubuyu’ huo, Ijumaa Wikienda
lilimvutia waya Lulu ambapo awali alidai hakumuona msibani hapo, lakini
baadaye alikiri kumuona ila hakupata fursa ya kumsalimia naye.
Post a Comment Blogger Facebook