Mayasa Mariwata
Staa wa nyimbo za Injili ambaye pia ni mwigizaji wa sinema za Kibongo, Sarah Mvungi amefunguka juu ya mwimbaji mwenzake, Rose Muhando kutaka kuhama Ukristo na kurudi kwenye Uislam
Akibonga na Ijumaa Wikienda,
wikiendi iliyopita, Sarah alistaajabu kauli ya Rose kuwa tangu amekuwa
Mkristo amekuwa akiandamwa na misukosuko mingi kiasi cha kukata tamaa na
kutamani kurejea kwenye dini yake ya awali ya Uislam.
“Rose hajielewi, anapaswa kumlilia
Mungu ili amuepushe na yanayomsibu (tuhuma za utapeli). Kuhamahama dini
ni sawa na kumchezea Mungu au pengine neno halikumuiingia vizuri,”
alisema Sarah. Jitihada za kumpata Rose ili kuzungumzia ishu hiyo
zikigonga mwamba.
Post a Comment Blogger Facebook