0
ILIPOISHIA..…….

“nakupenda Alex.”

Fridah aliongea kwa sauti ya kimahaba tulipokuwa tumekumbatiana huku maji ya bomba la mvua yakitumwagikia  mwilini.

“hata mimi nakupenda.”

Nilimuitikia .

Tulikuwa tumeshajisahau kabisa kwamba penzi letu ni la kuibia tu, na wala si rasmi kiasi cha kupendana kama sisi tuilivyokuwa tunafanya.kila mmoja alikuwa na mpenzi wake na wapenzi wetu walitupenda si mchezo.

Baada ya hapo tulitoka katika bafu hilo huku kila mmoja akimfuta mwenzake kwa taulo.

MUENDELEZO WAKE:

Tulipo maliza mambo yetu pale hotelini kila mmoja aliondoka kivyake mimi nilirudi zangu ofisini alafu yeye alienda wapi sijui.

Wafanyakazi wangu walijua labda nilikuwa nimeenda bandarini kufuatilia mzigo kumbe wapi nilikuwa jengo la pili tu kutoka ofisini kwangu.

Kusema kweli kitendo cha kufanya mapenzi na Fridah kilileta mabadiliko makubwa sana kwangu. Sikuwa Yule mwanaume ambaye mara baada ya kutoka kazini alikimbia mbio mbio kwenda kuyaminya minya matako ya mwanamke wake. Bali Yule anayeibua vikao feki na miahadi ya wafanyabishara wanzake kila ifikapo jioni ili mradi tu amtoroke mwanamke wake na kwenda kuponda raha na kimada.

Huo ndio ulikuwa ukweli, jimama enjol alishindwa kunielewa kabisa msimu huu, na kila alipotaka kunidadisi nilikuwa mkali.

Karani nae alinipigia simu na kuniomba tukutane, sikumkatalia , natullipokutana hakuwa na lolote la kusema zaidi ya kuniomba niachane na Fridah.

“mbona sikuelewi Karani , toka lini mimi nimekuwa na uhusianao na Fridah.”

“Mimi najua , Alex ninawajua wanawake fika , mwanamke hawezi kubadilika ghafla hivi kama hana mwanaume mwingine na yote yameanza tangu siku ile tulipokutana pale hotelini.”

Aliongea karani kwa uchungu.

“hicho sio kigezo karani na wala haimaanishi kama ana mwanaume mwingine basi lazima niwe mimi, na anaweza asiwe na mwanaume akawa ametingwa  na kazi tu.”

“kazi  wapi , kila siku anafanya kazi lakini kamwe hajawahi kuniambia hawezi, kufanya mapenzi na mimi kwa wakati huo eti kisa amechoka .  nakwambia siku hizi tunalala mzungu wa nne sasa maisha gani hayo ndugu yangu.”

“mimi sifahamu lolote Karani, unaniuliza kitu ambacho ni kigeni kwangu.”

“Acha hizo Alex, jaribu kuwa binadamu mdogo wangu, mweenzako maisha yangu yote namtegemea Fridah , yani uhusiano wetu ukiharibika zaidi sijui ntaishi wapi mimi sina kibanda cha kujiegesha.”

Aliongea Karani maneno ambayo kusema kweli yalikuwa yakihuzunisha sana .

Kusema kweli nilimuonea huruma sana , nilitamani kumsaidia lakini kusema kweli sikuwa na jinsi  ilinibidi nikatae kata kata kwamba ninauhusiano na Fridah , kwani kama ningekubali basi hadi jimama enjol  angejua.

Na songombingo lake sijui lingekuwaje.

Karani alikuwa ni mmoja kati ya wanaume wazembe niliowahi kukutana nao katika maisha yangu.

Pamoja na  kutembe as na wanawake wote wale wenye nafasi  , aliokuwa akijitapa kwangu lakini leo anadiriki kuniambia kwamba hana hata kibanda cha kujisikiza.

Mara kadhaa Fridah aliniambia stori zake , kwamba alipomwambia amfungulie biashra karani alikataa na  akawa amelizika kukaa nyumbani kutunza bustani ya maua iliyopo katika nyumba hiyo na kumsubiri Fridaha atoke kazini ili afanye nae mapenzi.

                               ***

Nilifanya kazi ya kubadili viwanja na Fridah tena viwanja vikubwa vikubwa mara serena , sea cliff na kwengineko.  Huko Fridah alinikutanisha na marafiki zake mbali mbali waliokuwa na hadhi ya juu hata kuliko jimama Enjol , na wala hata walikuwa hawajui kwamba Fridah alikuwa na rafiki aliyekuwa akiitwa Enjol.

Lugha tuliyokuwa tukitumia kuongea  na marafiki zake hawa ni kizungu na kifaransa , kwa bahati nzuri nilikuwa napenda kucheza na lugha tangu nikiwa shule hivyo nilifiti kabisa .

Watu wote tuliokutana nao huko walijua kwamba mimi ndio mume wa Fridah.

Kusema kweli karan, kamwe asingeweza kufika viwanja hivi hata iweje.

Aliishia kupiga simu na kupata majibu ya mtumiaji wa simu unayompigia sasa hapatikani. Na hata kwa jimama enjol ilikuwa hivyo hivyo nae alipojaribu kunipigia.

Kilichonifurahisha ni ni tabia ya Fridah kunitambulisha kwa mashosti zake na wengi weao walikuwa wanajua habari zangu wakisema wamesikia mengi kuhusu mimi.

Sikujua hayo mengi waliyokuwa wakiyazungumzia ni kuhusu nini ila siku moja tulipomtembeleaa rafiki yake mmoja kwenye bangaloo lake ndipo niliujua ukweli pale Fridah alipoenda bafuni na kuniacha mimi na rafiki yake huyo peke yetu pale sebuleni.

Ameniambia kwamba unafanya mapenzi vizuri sana,  vipi kama na mimi nikionja huo utamu wa penzi lako, nitakupachochote unachotaka.”

Aliongea msichana huyo jambo ambalo lilinishtua kidogo, lakini pale alipoanza kuvitaja vitu ambavyo angeeza kunipa nilianza kulichukualia suala hilo pasipo mzaha .

Niliigundua kitu kimoja siku hiyo, kwamba mapenzi yanaweza kunifanya nikatajirika ghafla.

Mwanamke huyu alikuwa akizungumzia kunilipa kama milioni nne hivi za kitanzania kama nikikubali kufanya nae mapenzi, haikuwa pesa kubwa sana kwangu kwa wakati huo lakini nilipiga hesabu muda nitakao utumia kuipata pesa hiyo siyo sawa na muda ambao ningeipata katika mazingira ya kawaida .

Nilichokifanya mara baada ya hapo ni kukubaliana nae kisha tukapanga muda wetu wa siri na kufanya mapenzi na kweli alinipa pesa hizo na alifurahi kweli na akaniomba siku nyingine nitakapo pigiwa simu nisimuangushe.

Siku ya pili nilipokea simu nilipopokea nilisikia sauti ya kizungu  niliopoyasikiliza maelezo yake alidai amepewa namba yangu na Yule dada niliyefanya nae mapenzi jana. Alichoniambia mwanamke huyo wala sikuamini. Nae pia alikuwa anataka huduma ile kama niliyompatia mwenzake na alikuwa yupo tayari kulipa kiasi kile kile cha pesa milioni nne za kitanzania.

Kusema kweli ingeniwia vigumu kuukosa mkwanja mrefu kiasi hicho. sikuwa  na jinsi zaidi ya kumkubalia mwanamke huyo , alinielekeza nyumbani kwake nikaenda na kumkaza .

Ilipofika jioni nilipokea simu nyingine huyu nae alikuwa anataka huduma hiyo hiyo uya kukazwa.

Nilibaki nashangaa, nikawa sielewi kinachoendelea kwangu , haukupita hata muda mrefu simu yangu ikawa bize kweli kweli, nilikuwa mtu wa kubadilisha nyumba za watu tu utafikiri fundi bomba.

Sikumbi mara ya mwisho kulala nyumbani kwangu ilikuwa lini, jimama enjol pamoja na Fridah walikuwa wakinipigia simu wala nilikuwa sipokei , na wala sikurudi tena nyumbani kwangu badala yake nikaanzisha makazi mengine katika apartment maeneo ya mikocheni.

Na  hiyo hiyo ndio ikawa ofisi yangu, nilikuwa nikishinda ndani nikifanya mazoezi , nikiangallia ponografia na kusoma vitabu mbali mbali vya kielektroniki vinavyo elezea namna yakumridhisha mwanamke kimapenzi.

Lengo langu lilikuwa ni kufanya mapenzi katika kiwango cha kimataifa , kwa sababu sasa nilikuwa nikifanya mapenzi na wanawake kutoka sehemu mbali mbali ulimwenguni.

 Na wala haikuwa mara moja kwangu kupokea simu kutoka nchi mbali mbali wakinitaka niwafuate nchini kwao . kusema kweli nilizipenda mechi nilizopata nchi za nje kwa kuwa  malipo yake yalikuwa makubwa zaidi na nikiwa huko huwa nilikuwa nabahatika kuunganisha mechi 20 mpaka 50 kabla sijarejea nyumbani.

Haikupita hata miezi sita nilijikuta nina mkwanja mrefu hatari, nikafungua ofisi ya duka la nguo lakini hili lilikuwa kubwa zaidi ya lile ambalo alinipa jimama enjol, ambalo sijui hata linaendelea vipi.

Nilikuwa na mkwanja wa mrefu sana , kwa mara ya kwanza niliwatembelea wazazi wangu ambao walikuwa wakidhani nipo mkoani hadi wakati huo. hawakuamini kile walichokiona , kila kitu walichokiona kwangu kiliwashangaza.

Nilimletea baba yangu zawadi ya gari la kutembelea  na niliwashangaza pale nilipowaaambia kwamba nataka kuibomoa nyumba hiyo niwajengee upya nyumba ya kisasa.

Familia nzima niliipeleka hotelini wakawa wanakaa kusubiri ujenzi wa nyumba ukamilike , ilikuwa vigumu kuwapeleka nyumbani kwangu kwa sababu ya kazi yangu, kwani wakati mwingine wanawake walinifuata nyumbani kwangu na ilibidi niwahudumie hapo hapo , hususani wake za watu ambao walikuwa wakihofia wanaume zao kujua kwamba wanachepuka.


Itaendelea……

Post a Comment Blogger

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();
 
Top