0
ILIPOISHIA..…….
Aliingia chumbani na kisha kutoka na miwani myeusi. Kweli niliiona kwenye meza ya kioo lakini sikujua kwamba imewekwa kwa ajili yangu.
Nilipoivaa miwani hiyo enjol ndio alinisifia zaidi.
Baada ya hapo tulitoka na gari yake , breki ya kwanza ilikuwa kwenye saluni moja kubwa iliyopo katikati ya jiji hapo wataalamu wa nywele na kung’arisha sura kwa kusuisugua walinishughulikia nabaada ya  hapo uzuri wangu ulionekana haswa, nilikuwa niking’aa yaani.
Hata mimi mwenyewe nilipojiangalia kwenye kioo cha saluni hiyo nilibaki najishangaa.
Unaweza sema labda sio mimi ni mtu ninaye fanana naye ambaye maisha yake yote amekuwa akiiishi merekani.
Kumbe hapa hapa bongo dar es salaaaam.

MUENDELEZO WAKE…..
Tulipotoka kwenye saluni hiyo Jimama Enjol alinipeleka mpaka kwenye duka moja la nguo lililopo kati kati ya jiji, mimi nilijua sasa tunaenda kuchagua nguo nilijiweka sawa kwa ajili ya kuchagua mikato yangu nikajua sasa itakuwa ile ndoto ambayo jimama enjol alisema inaweza kutimia nafikiri ndio hii.
Lakini kilichotokea hapo unajua mara baada ya kuingia ndani ya duka hilo wafanyakazi wa duka hilo wote walikuwa wakimtetemekea , aliwaita wote na kunitambulisha wote kwangu .
“kuanzia leo huyu ndio atakuwa bosi wenu hapa.”
Aliongea Jimama enjol huku akinishika bega , kwa kweli sikuamini kabisa kile nilichokisikia.
Kusema kweli hii ilikuwa zaidi ya ndoto yangu.
“Alex, hili ni duka lako tangu sasa.”
Aliongea Jimama Enjol na kuzidi kunifanya nipagawe , nilijua kwamba anaweza kuninunulia pamba  za kila aina , lakini kunikabithi duka zima lenye wafanya watano. Hii ilikuwa ni ndoto kwa kweli.
Jimama enjol hakuishia hapo alinipeleka sehemu nyingine kwenye nyumba moja ya kifahari, nilifikiri tunaenda kumtembelea rafiki yake au mtu Fulani lakini tulipoingia ndani ya nyumbna hiyo akanimaliza nguvu pale aliposema hii ni nyumba yako na lile gari tuliloliona limepakiwa kwenye maegesho ya nyumba hii ndilo gari lako.
Na kwambia ukweli nilikuwa kama mwenda wazimu siku hiyo, nilishinndwa hata niseme nini , nilijikuta napiga kelele na kushangilia kama mwenda wazimu, hii ilikuwa zaidi ya kila nilichokuwa nikikiota katika maisha yangu,  mwanamke huyu amebadilishakila kitu katika maisha yangu , mpaka nilijikuta namuogopa.
“kwa nini umefanya yote haya kwangu, Enjol?”
Nilimuuliza .
“unastahili haya, Alex, niamini mimi yani kwa kazi unayoifanya nahisi hata yote haya niliyoyafanya kwako ni madogo, unanifanya nifurahie maisha Alex, hakuna mtu anayefanya mapenzi kama unavyofanya wewe, unakipaji cha kufanya mapenzi, natakiwa kukupa heshima yako.”
Aliongea Enjol maneno ambayo kwa kweli sijui hata alikuwa anayatoa wapi, bado mimi nilimuona mtu wa ajabu, mambo yote haya alinipatia eti kwa sababu ninamkuna vizuri kitandani, bado ilikuwa ainiingii akilini kabisa.
Tulikaa hapo kwa muda Fulani katika jumba hilo la kifahari lenye kila kitu unachokijua wewe kinachokuwemo katika nyumba. baada ya muda Fulani , kengele ya nyumba hiyo iligongwa .
“atakuwa nani tena huyo?”
Niliuliza kwa mshangao .
“kuna mtu nilikuwa na mtarajia usiwe na wasi wasi Alex.”
Aliongea Jimama enjol na kisha kwenda kumkaribisha mtu huyo.
Aliporudi nilishangaa kumuona akiwa ameongozana na mchina.
“na huyo ni nani?”
Niliuliza kwa mshangao.
“huyu ni Shi yuu, yeye atakuwa mwalimu wako wa kung fu.”
“kung fu!”
“ndio, Alex maisha yako yamekwisha badilika sasa , umeshakuwa mtu wa hadhi ya nyota tano, lazima ujue jinsi ya kujilinda mwenyewe , sipendi mpenzi wangu uwe katika hatari alafu ushindwe kujiokoa mwenyewe.”
Aliongea jimama enjol huku akiniangalia.
Kwa kweli kila nikimuangalia Enjol sikuweza kumuelewa kabisa , kila kitu alichokuwa akikifanya kwangu kilikuwa ni zaidi.
“mpenzi unaaanza kushughulika na mamilioni sasa hivi , unafikiri majambazi hawatakuwa wanakutolea macho? Hata hivyo nimeshakuandalia fomu yakujaza ili umiliki bastola yako, ukimaliza mafunzo haya utaanza kujifunza kulenga shabaha , umenielewa mpenzi.”
“nimekuelewa.”
Niliitikia na kisha kumvuta na kumbusu , mbele ya huyo shi yuu nani siijui wa kichina .
“honey , subiri kidogo basi, tumalizane na mgeni mmmh”
Enjol aliongea kwa sauti ya chini huku akijaribu kunizuia lakini utamu wa busu langu ulikuwa haukwepeki. Huku akisita sita alijikuta analeta mdomo wake na mimi niliudaka na kuanza kumnyonya denda.
Shi yuu, alikuwa ameketi sofani akituangalia kwa jicho la wizi wizi.
Enjol alitamani kunizuia , kwa sababu alikuwa akieshimiana na mr shii yuu, lakini alinogewa na utamu wa denda nililokuwa nikimpatia.
“I love you Alex “
Aliongea enjol akiwa amenikumbatia .
kisha tulishitisha zoezi hilo na kumgeukia mr shi yuu.
“we are  sorry  for every thing mr shii”
[tusamehe kwa kila kitu bw. Shii.]
“nonono , love  is good , I can wait more than this if it is about love.”
[ hapana , hapana , hapana , mapenzi ni mazuri , naweza kusubiri zaidi ya hivi kama ni juu ya mapenzi.]
Aliongea mchina huyo kisha wote tulicheka .
“I have been wait for fiftin years to see my wife in china can you imagine?”
[nimesubiri kwa miaka kumi na tano kwenda kumuona mke wangu nchini china unaweza kuvuta picha?]
Aliongea bw. Shii yuu kwa  hisia. sote tulimwangalia na kumuonea huruma , kwa jinsi alivyokuwa akiongea alionekana mwenye hamu kubwa ya kumuona mke wake.
“why you spend all these years without seeing her?”
[ kwanini umekaa miaka yote hiyo pasipo kumuona?]
“family problem , her father is a mafia , he want to use me in his dirt job since he knew that I have good kung fu, so I had to run, and Africa is only place where he can’t track.”
[ Matatizo ya kifamilia , baba yake ni mafia, alitaka kunitumia mimi katika kazi zake chafu baada ya kujua kwamba naweza kupigana vizuri kungfu, kwa hiyo nilikimbia , na afrika ndio sehemu pekee ambayo hawezi kuipata. ]
Alimaliza kuongea shii yuu huku machozi yakimlenga machoni, huruma ilitujaa sote.
“pole sana.”
Enjol alimwambia.
“ahsante’
Aliitikia bw shi yuu.
Maongezi yetu yaliishia hapo kilichofuata ilikuwa ni kupeana ratiba ya muda wa kuanza kufanya mazoezi.
Shi yuu alitakiwa kuwasili nyumbani kwangu kila siku alfajiri  kuanzi siku inayofuatia .
Huwezi kuamini siku hiyo hata habari ya kwenda nyumbani sikuifikiria nilichokifanya ni kuwa pigia simu na kuwaambia nimepata dili la mikoani kwa hiyo nitasafiri kwa miezi kadhaa.
Aliponiuliza mkoa gani nikawaeleza nitazunguka mikoa mbali mbali lakini kwa sasa naelekea mwanza.
Na hivyo ndiyo nilivyoagana na familia yangu.
Na hapo sasa ratiba yangu yote ilibadilika niliamka alfajiri kila siku kwa ajili ya kufanya mazoezi ya kungfu na Shi yuu, kisha mida saaa mbili nilikwenda kusimamia duka langu, na jioni kabla ya kupata chakula cha jioni na Enjol nilikuwa na somo langu la siri ambalo nililifanya mwenyewe.
Nilifungua kila mtandao na kusaka karibu kila kitabu kinachozungumiza jinsi ya kumfanya mwanamke alidhike kimapenzi, kama sutra na vingine vingi, kila aina staili kila aina ya mapenzi katika tamaduni mbali mbali duniani kote, pamoja na kuangalia porno za kutoka sehemu mbali mbali ulimwenguni , na kila siku Enjol alipokuja nilikuwa nikifanyia mazoezi yale niliyojifunza, jambo ambalo lilimfanya azidi kupagwa kimapenzi na mimi , alibaki akiduwaa kila siku anapakuliwa chakula kipya , yani hadi akawa kama mwenda wazimu , kuna wakati alishindwa kuvumilia na kunifuata ofisini akitaka tufanye mapenzi humo humo , wafanyakazi wote walitoka nje na duka lilifungwa kwa muda na pale tulipomaliza kufanya mambo yetu , Enjol aliondoka na kisha duka lilifunguliwa.

inaendelea  giftkipapa.com

Post a Comment Blogger

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();
 
Top