Mwanafunzi
 wa kidato cha pili wa Sekondari ya Nyasubi, Ally Jacob ameuawa baada 
kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni alipokuwa akijaribu kumwokoa 
mwanafunzi mwenzake asibakwe.
Tukio
 hilo lilitokea juzi saa 9:00 alasiri maeneo ya Nyasubi, Wilaya ya 
Kahama mkoani Shinyanga. alikuwa akirejea nyumbani kutokea shuleni.
Kamanda
 wa Polisi mkoani Shinyanga, Justus Kamugisha alidai kuwa mwanafunzi 
huyo aliuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya shingoni na
 mwenzake anayesoma Sekondari ya Kishimba.
Kamugisha
 alisema sababu za Jacob kuuawa ni kujaribu kumsaidia mwanafunzi 
mwenzake mwenye umri wa miaka 16 (jina linahifadhiwa) ambaye anasoma 
kidato cha pili Sekondari ya Nyasubi ili asibakwe na mtuhumiwa ambaye 
alitaka kufanya unyama huo kwa kushirikiana na mkazi mmoja wa Nyasubi.
Alisema watuhumiwa wote wamekamatwa na watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Post a Comment Blogger Facebook