
Polisi
 nchini imepiga marufuku vikundi vya ulinzi vya vyama vya kisiasa , 
vyenye mwelekeo wa kijeshi kufanya kazi za ulinzi hadharani kwa madai 
kuwa vinaingilia majukumu yao.
Onyo
 hilo lilitolewa jana na Kamishna wa Polisi–Operesheni na Mfunzo, Paul 
Chagonja wakati akizungumza na waaandishi wa habari Makao Makuu ya 
Polisi, Dar es Salaam.
Chagonja
 alivitaja vikundi hivyo na vyama vyao kwenye mabano kuwa ni Green Guard
 (CCM), Red Brigade (Chadema) na Blue Guard (CUF), ambavyo hutumiwa na 
vyama vya siasa hususan katika mikutano yao.
Agizo
 la Chagonja limekuja ikiwa ni miezi minne baada ya agizo la Mkuu wa 
Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Ernest Mangu 
kupiga marufuku vikundi hivyo vya vyama vya siasa ambavyo vina muonekano
 na muundo wa vyombo vya usalama, kwani ni kinyume cha katiba na sheria 
ya nchi.
Alivitaka
 vyama hivyo kuhakikisha vinafuata muongozo uliotolewa na Ofisi ya 
Msajili wa vyama hivyo na kama vikienda kinyume jeshi litapambana navyo.
IGP
 Mangu aliyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa Baraza la 
Vyama vya Siasa, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Polisi uliokuwa 
ukijadili namna ya kuondoa vikundi hivyo pamoja na namna ya kuboresha 
shughuli za uendeshwaji wa vikundi hivyo.
Alisema
 vikundi hivyo vipo kinyume cha sheria na kwamba kuendelea kuvimiliki 
kwa kisingizio chochote ni uvunjifu wa Katiba ya nchi na sheria ya vyama
 siasa, jambo ambalo polisi haliwezi kulivumilia.
“Polisi
 imejipanga vizuri kuhakikisha mikutano ya kampeni ya vyama vya siasa 
inafanyika katika hali ya utulivu hadi siku ya uchaguzi,“ alisema 
Kamishna Chagonja.
Alisema
 katika kipindi cha kuelekea katika kampeni zinazoanza leo ni muhimu 
kila mmoja kujiepusha na makosa yanayoweza kupelekea jinai.
Huku akitoa mfano wa makosa hayo ni kubandua picha ya mgombea wa chama fulani kinyume cha sheria.
Kamishna
 Changonja aliwakumbusha wagombea kwa nafasi zao kuwaelimisha wafauasi 
wao umuhimu wa kuheshimu sheria ili kudumisha amani, usalama na utulivu 
katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi.
“Tunatoa
 tahadhari kwa wananchi pia kuzingatia sheria zinazowaongozwa ikiwamo 
sheria ya vyama vya uchaguzi na miongozo mbalimbali iliyotolewa na 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),” alisema Chagonja.
Akizungumza
 hatua hiyo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa askari 
polisi hawatoshi kulinda mkutano wa watu wengi hivyo wataendelea 
kuwatumia kulinda wanachama wao.
Naye
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema katika chama 
chao hakuna kikundi kinachoitwa Green Guard kwani hata Katiba ya chama 
hicho hakina watu kama hao.
Mkurugenzi
 wa uchaguzi wa Chama cha CUF, Shaweji Mketo alisisitiza chama chake 
kuendelea kuwatumia, kwa sababu wapo kikatiba na katiba yao ilipitishwa 
na Serikali na inatambuliwa na msajili wa vyama vya siasa.
Kwa
 mujibu wa Mketo, kauli ya Chagonja ni kutaka wavunje katiba ya chama, 
kwani maamuzi ya kuwatumia yalipitishwa na mkutano mkuu, “Tutawatumia 
hiyo ya kutukataza haipo, wapo na katiba ya chama iliweka hilo na 
msajili wa vyama vya siasa akalipitisha hilo, ina maana hakuona tatizo, 
”alisema.
Alifafanua
 kuwa Red Guard hawajawahi kusababisha matatizo zaidi ya kulinda amani, 
hivyo hawana sababu ya msingi ya kuacha kuwatumia. Mketo alilalama kuwa 
kila unapofika uchaguzi kunakuwa na kauli za kukatisha tamaa na 
kutishwa, wao hawaogopi kwa sababu wamefuata sheria.
kutoka 
Mpekuzi blog
Mpekuzi blog
Post a Comment Blogger Facebook