
Machemli,
aliyekuwa Mbunge wa Ukerewe mkoani Mwanza, alijikuta akishindwa kupata
kura za kutosha katika uchaguzi huo uliofanyika juzi mjini Nansio,
Ukerewe.
Awali,
uongozi wa Chadema Makao Makuu ulikuwa na mapendekezo kwamba wabunge wa
majimbo wa chama hicho wapite bila kupingwa na ingawa wengi walikuwa na
wapinzani, wamefanikiwa kuvuka kizingizi cha kura za maoni isipokuwa
Machemli.
Aliyembwaga
Machemli ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Joseph Mkundi,
aliyepata kura 232 kati ya 466 zilizopigwa, akiwashinda wagombea wengine
tisa huku Machemli akiambulia kura 74.
Post a Comment Blogger Facebook