Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

Wednesday, July 12, 2017

Imevuja: Yanga Kumsajili Erasto Nyoni

KIUNGO anayeweza kucheza nafasi zote za ulinzi, Erasto Edward Nyoni yuko mbioni kujiunga na mabingwa wa Tanzania, Yanga baada ya kumaliza mkataba wake Azam FC

Nyoni yupo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayojiandaa kwa mchezo na Rwanda Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza kuwania tiketi ya Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), michuano inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee – na Yanga wanatarajia kumalizana naye kabisa baada ya mechi hiyo.

“Mazungumzo na Nyoni yamekwenda vizuri na wakati wowote tunaweza kumalizana naye, pengine baada ya mechi tu dhidi ya Rwanda,”kimesema chanzo kutoka Yanga.

Benchi la Ufundi la Yanga, chini ya Kocha Mkuu, Mzambia George Lwandamina kwa kushirikiana na Sekretarieti chini ya Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa ambaye kitaaluma ni kocha kwa pamoja wamejiridhisha Nyoni ni mchezaji ambaye wanamuhitaji kikosini.

Na hiyo ni kwa sababu huyo ni ‘kiraka’ anayeweza kucheza nafasi yoyote ya ulinzi kuanzia kiungo wa ulinzi – lakini uzoefu na weledi wake kisoka ni vitu vingine vinavyomuunganisha na Yanga katika siku za mwishoni za maisha yake ya uwanjani

Everton inafungulia Milango Tanzania - Mwakyembe

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe amesema ujio wa timu ya Everton nchini utaweza kufungua fursa nyingi kwa kuwa dunia nzima sasa itaitazama Tanzania kupitia mchezo kirafiki dhidi ya Gor Mahia.


Mwakyembe amebainisha hayo muda mchache alipoupokea ugeni huo huku akizisisitizia timu za Tanzania kutumia viwanja vilivyopo nchini vizuri ili waweze kuinua vipaji kwa hali ya juu.
"Hii ni fursa kubwa kwa watanzania kwanza kuwaona hawa nyota wa Everton ni timu kongwe kutoka Uingereza lakini pili inafungua fursa sana maana inatutangaza watanzania kidunia, wamekuja na watangazaji kutoka nchi mbalimbali. Kwa hiyo inafungua milango kwa timu nyingi zaidi, nasi tuzishawishi zaidi timu zetu zije kutumia viwanja vyetu vya kisasa tulivyo navyo", amesema Mwakyembe.

Pamoja na hayo, Mwakyembe amewatuliza wanahabari pamoja na wapenzi wa soka kuwa na moyo wa uvumilivu kwa kuwa hawataweza kupata nafasi ya kukiona kikosi hicho kikiwa kinafanya mazoezi yake kwa ajili ya mchezo wa kesho dhidi ya Gor Mahia ya Kenya kutokana na kuwepo na ulinzi mkali.

"Nafikiri kesho kutakuwa na mchezo mzuri kweli, leo watafanya mazoezi katika uwanja Taifa lakini naona wenzetu hawataki kabisa kuona vyombo vya habari pale, hatuwezi kuwapinga kwa hilo. Kwa hiyo vijana wangu msihangaike hata kwenda pale maana kuna ulinzi mkali lakini kesho nitahakikisha kila mmoja wenu anapata nafasi nzuri kuweza kufuatilia mchezo huo jioni", amesisitiza Mwakyembe.

Everton itashuka dimbani kesho (Alhamis) kuchapana na Gor Mahia mchezo wa kirafiki baada ya kuibuka kuwa mshindi wa kwanza wa michuano ya Sportpesa Super Cup 2017

Duh.. Afande Sele Amuombea Mabaya Aliyekuwa Rais wa TFF...Acha Magufuli Awanyooshe

Msanii mkongwe wa Hip hop nchini Afande Sele amefunguka na kumuombea mabaya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi na kusema ni bora aende kwani katika kipindi chake hakuna jambo lolote la maendeleo amelifanya.

Afande Sele ametumia ukurasa wake wa facebook na kusema yake ya moyoni kwa kulinganisha ofisi na hatua ambazo zimepigwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Sudan na kusema Malinzi anapaswa kuondoka tu kwani ni aibu.

"Ofisi ya chama cha soka cha Sudan na ofisi ya chama cha soka Tanzania..aibu yetu..acha Magufuli atunyooshe tu kwani tulizidisha uwendawazimu. Nenda Malinzi nenda tuuu" alisisitiza Afande Sele

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi ambaye alikuwa ni mmoja kati ya watu ambao walikuwa wanagombea nafasi ya Urais katika shirikisho hilo lakini jina lake lilienguliwa katika mchakato huo baada ya kushindwa kuhudhuria katika usaili wa wagombea uliofanyika siku ambayo yeye yupo rumande kutokana na kesi inayomkabili ya matumizi mabaya ya ofisi.

Friday, September 23, 2016

wazee wa mikeka 23/09/2016

Inter vs Bologna

pick inter milan win odds 1.60
result?

Toulouse vs Paris SG

pick PSG  win   odds 1.40
result 
Dortmund vs SC Freiburg
pick Dortmund win odds 1.20
pick Dortmund home team goals over 2.5 odds 2.01
pick Dortmund AsianHandicap -2.0  odds 1.95


Shebourne v Limerick
pick over 2.5 goals  odds 1.55


Manchester City U23 v Leicester City U23
pick Man City win odds 1.40

Finn Harps vs St Patrick's Athletic
Pick St patrick win  odds 1.85



Friday, September 16, 2016

Ubashiri wa baadhi ya mechi za leo... 16/09/2016

1.Wexford vs Derry City
Derry City leo watakuwa ugenini  Ferrycarrig  kujihakikishia nafasi ya tatu kwaka msimamo wa ligi ya ireland  kwa ushindi dhidi ya wexford youth ambao wanasua sua .. na wanapamba wasishuke daraja.. huku wexford youth  wakiwa wamepoteza michezo kumi kati ya 12 iliyopita 
na wakiwa wametoka kufungwa kwenye lig cup juma lililo isha na derry city 3-1 
leo derry city  wakimfunga tena wexford youth itakuwa ni ushindi wa nne mfululizo katika msimu huu...
mzigo wangu na uweka kwa 
Derry City odds 1.72
RESULT?

2.Achilles '29 vs Telstar
achilles
achiles29 wanashika mkia katika ligi daraja la pili nchini uholanzi, wakiwa wamecheza michezo saba na kushinda mmoja pia ikiwa ni timu ambayo haijatoa clean sheet katika michezo yake 12 iliyopia leo wanakutana na telstar inayohitaji matokeo....ili kujiweka katika nafasi nzuri katika ligi
mechi hii naamini itakuwa na zaidi ya magoli matatu na pia watafungana...
mzigo wangu ni kwa 
Telstar DNB odds 1.78
GG&3+ odds 3.55
Telstar -0.5 AH odds 2.60
RESULT Achilles'29 1-2 Telster

Thursday, September 15, 2016

Ubashiri wa baadhi ya mechi za leo....

baada ya jana kuanza vizuri.. leo tunaendelea....

1. Konyaspor v Shakhtar Donetsk
baada ya kutolewa kwenye champions league qualifiers Shaktar wamegeuzia nguvu zao kwenye Europa league kikosi kipo sawa na wameanza ligi vizur bila shaka ushindi leo ni wa muhimu maana ugenini ni kama nyumbani.... kwa sababu hata za nyumbani wanachezea kiwanja tofauti na cha kwao... konyaspor hawana nguvu ya kumzuia shaktar kutopata matokeo
  mzigo wangu ni ushindi kwa
Shaktar Donetsk odds 1.78
Konyaspor 0-1Shakhtar Donetsk WON

2. Feyenoord vs Man Utd

fayenoord leo wanakibarua kigumu katika europa league dhidi ya Man utd chini ya Jose Mourinho japokuwa wameanza ligi vizuri na ushindi mara tano mfulilizo
man Utd watakuwepo bila ya Rooney na luke shay pamoja na phil jones pia tutategemea Rashford kuanza mechi ya leo nategemea Man Utd kuchukulia hii game seriously kwa hiyo ushind utakuwa ni lazima kutokana na kufungwa na Man Cty jumamosi watahitaji.. kubounce back kama walivyo fanya Leicester City na Barcelona na Dortmund
Mzigo wangu na uweka kwa
Manchester United odds 1.85
Manchester United AH -0.5 odds 2.05
RESULT
Fayenoord 1- 0 Manchester United LOSE

3.Southampton vs Sparta Prague
southampton pamoja na kuanza vibaya msimu haimanishi wao ni wabovu...sana  kama wakicheza sawa sawa na walivyo cheza mechi yao ya jumamosi dhidi Ya arsenal wana uhakika wa kushinda Mechi ya leo.... na ikichangiwa hawana majeruhi wapya nategemea  Thomas Rosicky na timu yake watakuwa na kibarua cha kuzuia na kutafuta angalau point moja....
mimi mzigo wangu nauweka kwa 
Southampton odds 1.65
wale wa Asian Handcap Southampton -0.5 AH  odds 1.92
RESULT
Southampton 3-0 Sparta praha WON

Friday, August 19, 2016

Olimpiki: Mwanariadha wa Kenya Apokonywa Medali Kwa Kosa la Udanganyifu

Mwanariadha kutoka nchini Kenya aliyeshinda medali ya shaba kwenye riadha na kuruka vihunzi pamoja na maji, Ezekiel Kemboi amepokonywa medali yake kwa kosa la udanganyifu mchezoni kwenye mashindano ya Olimpiki yanayoendelea huko nchini Brazil.

Kemboi (34) alimaliza kwenye nafasi ya tatu ya mashindano hayo ya kukimbia ya mita 3000 kwa kutumia muda wa 8:08.47. Ufaransa ilipinga ushindi huo wa Kemboi kwa kukata rufaa baada ya kubainika kuwa mwanariadha huyo wakati akiendelea na mbio hizo baada ya kuruka kiunzi na maji, alikanyaga nje ya mstari.

Kamati ya mashindano hayo imekubali rufaa hiyo na kuamuru kumpatia medali hiyo ya shaba, Mahiedine Mekhissi kutoka Ufaransa aliyeshika nafasi ya nne baada ya kukimbia kwa muda wa 8:11.52.

Hata hivyo Kemboi ambaye alikuwa bingwa wa mbio hizo kwenye mashindano ya Olimpiki ya 2012 ya nchini Uingereza amedaiwa kutangaza kustaafu kucheza mchezo huo

Friday, August 12, 2016

UBAHILI WA ARSENAL NA UBORA WA WAPINZANI WAO MSIMU WA 2016-17


Bahili
Na Mahmoud Rajab
“Hatuwezi kushindana au kwashinda washindani wetu ambao wana pesa nyingi kuliko sisi. Tunapaswa kuwa makiini sana, kufanya machaguo sahihi.”Hayo nia aina ya maneno ambayo kwa miaka kadhaa sasa wamekuwa wakisikia kutoka kwa kocha na viongozi wao juu ya wapinzani wao. Ni Arsenal wenyewe kupitia kwa Mkurugenzi Mtendaji wao Ivan Gazidis waliwaaminisha washabiki wa wapenzi wao kwamba, klabu ina akiba ya kiasi cha paundi mil 200 kwaajili ya usajili, hivyo wana uwezo wa kuleta mchezaji yeyote.
Bila kupepesa macho ni ukweli kwamba, Arsene Wenger ndiyo meneja bora tangu Herbert Chapman na ataacha historia kubwa pale atakapoondoka. Miaka ishirini ya kushiriki Ligi ya Mabingwa mfululizo yanabaki kuwa mafanikio makubwa kwake na klabu, makombe matatu ya Ligi ya England na sita ya FA bila kusahau kumaliza msimu wa ligi bila kupoteza mchezo ni jambo la kujivunia sana.
Hata hivyo, licha ya mambo yote hayo niliyotaja hapo juu ambayo ni ya kujivunia kwa klabu hiyo, Arsenal hawajatwaa taji la Ligi ya England kwa miaka 12 sasa, hawajavuka hatua ya 16 bora kwenye Uefa kwa miaka sita mfululizo na kuwa klabu pekee kwenye ligi kubwa tano Ulaya kutosajili mchezaji wa ndani kwenye dirisha usajili lililopita licha ya kuwa na uhitaji wa wachezaji.
Mwanzoni mwa dirisha hili alianza kuwahadaa washabiki na wapenzi wa Arsenal. Pengine alikuwa kocha wa kwanza miongoni mwa makocha wa vilabu vikubwa barani Ulaya kuanza kusajili baada ya kumsajili kiungo Granit Xhaka kutoka Borussia Monchengladbach kwa ada ya paundi mil 35, kabla ya kumuongeza kinda wa Kijapan Takuma Asano, beki Rob Holding (20) na kinda wa Kinigeria  Kelechi Nwakali (18). Na kwa namna inavyoonekana ni wachezaji Xhaka na Holding pekee ndio watakaokuwa kwenye kikosi cha kwanza msimu huu, huku Asano and Nwakali wakisubiri vibali vyao kwaajili ya kutolewa kwa mkopo kwa ili kupata uzoefu zaidi.
“Inabidi tufuate gharama zinazolipwa na watu wengine,” hivi karibuni Wenger alisema. “Bei zimekuwa juu sana kwasababu upatikanaji wa pesa uko juu sana. Na ndiyo maana unaona sasa tumevuka mpaka paundi mil 100 kwa usajili wa mchezaji mmoja tu.
“Tunataka kutumia pesa tulizonazo,” aliongeza. “Lakini tunaheshimu pia pesa tulizonazo, ni vigumu sana kupata wachezaji wenye ubora halisi kwenye soko la sasa. Licha ya uwepo wa pesa nyingi sana hapa England lakini bado utaona watu wanafanya usajili taratibu sana.
Hayo ndiyo maneno ya Arsene Wenger ambayo kila siku amekuwa akiyasema. Arsenal wanahitaji nini hasa? Wanahitaji beki wa kati mwenye uzoefu wa kutosha kusaidiana na Per Mertesacker, Laurent Koscielny pamoja na Gabriel Paulista. Wanahitaji mshambuliaji mwingine wa kusaidiana na Olivier Giroud. Giroud tayari ameshidndwa kuonesh kila ambacho wenzake kama Thierry Henry na Robin van Persie walionesha katika nyakati zao.
Ikumbukwe kwamba nyuma ya Giroud kuna fundi wa pasi Mesut Ozil ambaye msimu uliopita aliweka rekodi ya kutengeneza nafasi nyingi ikiwa ni pamoja na pasi za magoli. Sasa ili Ozil azidi kufanya kile wanachotarajia watu wengi, inahitajika straika mwingine wa kumpa changamoto Olivier Giroud na kutoa upinzani mkubwa kwa timu nyingine.
Kwa sasa Per Mertesacker and Gabriel Paulista watakuwa nje kutokana na kusumbuliwa na majeraha. Hii sasa imemlaziku Wenger kutoka kwenda kutafuta mbadala ambaye atazidi pengo hilo, na taarifa zilizopo zinadai kwamba Shkodran Mustafi anatajwa kumalizana na klabu hiyo hivi karibuni. Huyu walau atakuwa msaada mkubwa kutokana na ubora na uwezo wake wa kusoma mchezo, kitu ambacho Arsenal inahitaji kwa kiasi kikubwa kwa sasa.
Lakini wasiwasi unabaki kwamba, Je, Wenger ataleta mshambuliaji? Kushindikana kwa uhamisho wa Jamie Vardy na kuamua kubaki Leicester na kukataliwa kwa ofa yao ya kwanza ya paundi mil 29 na Lyon juu ya mshambuliaji Alexandre Lacazette ni mifano ya hai ya changamoto anayokumbana nayo Arsene Wenger kwenye nafasi ya ushambuliaji.
Siku 16, michezo mitano, nchi nne, magoli 17 ya kufunga na matano y kufungwa. Arsenal wamemaliza kwa namna hiyo msimu wao wa pre-season kufuatia safari zao kwenye nchi za Ufaransa, Marekani, Norway na Sweden. Walihitimisha mechi yao ya mwisho kwa ushindi mujarab wa magoli 3-2 dhidi ya Manchester City. Wameonekana kuimarika kwa kadri walivyozidi kucheza mechi zao za kirafiki.
Chuba Akpom ameonesha kuimarika baada ya kufunga kwenye michezo minne mfululizo. Ilielezwa kwamba angeweza kuanzishwa kwenye mchezo dhidi ya Liverpool lakini kiwango kizuri cha Walcott kwenye mechi mbili dhidi ya Viking FK na Manchester City kunaweza kusababisha aanze badala ya Akpom. Hata hivyo kwa jinsi hali ilivyo bado anahitajika straika mwingine mwenye ‘killer instincts’, Akpom bado hana uzoefu wa kutosha.
Ujio wa makocha kama Pep Guardiola, Jose Mourinho na Antonio Conte, jumlisha usajili wa wachezaji kama Zlatan Ibrahimovic, Paul Pogba, Ilkay Gundogan na N’Golo Kante, Arsenal watakuwa na kibarua kigumu sana msimu huu kwenye mbio za kuwania taji la EPL. Kwenye mchezo dhidi ya Liverpool watakuwa na wasiwasi mkubwa pale safu yao ya ulinzi itakapokuwa chini ya makinda wasio na uzoefu Rob Holding and Calum Chambers, huku mapema kabisa wakianza kuandamwa na mkosi wa majeruhi.
Kuna wasiwasi wa utimamu wa Santi Cazorla ambaye ametoka kuuguza majeraha yake ya goti bila kusahau spana mkononi Jack Wilshere ambaue pamoja na kutocheza kwa muda mrefu, majeraha yamekuwa sehemu ya maisha yake na sasa anasumbuliwa na maumivu ya goti.
Msimu huu ambao unaonekana kuwa na ushindani mkubwa zaidi kuwahi kutokea baada ya kipindi kirefu, unaweza kushuhudia Arsenal wakiangukia pabaya zaidi kama hawataenda na upepo unavyotaka. Bado kuna muda mwingi tu wa usajili, na kama Arsene Wenger akiendelea kubania pesa za usajili ama hakika anaweza kuandika historia mpya, huku akiwa anaelekea ukingoni mwa mkataba wake

ujumbe wa basti schweinsteiger kwa mashabiki wa united

Bastian 13
Bastian Schweinsteiger amesisitiza kwamba bado ana furaha kuishi jijini Manchester licha ya kutojumuishwa kwenye kikosi cha timu hiyo na kocha Jose Mourinho.
Mjerumani huyo ameondolewa na kuwekwa kwenye kikosi cha akiba na kocha Jose Mourinho, ambaye alithibitisha kwamba haihitaji tena huduma ya Schweinsteiger
Anatarajiwa kuondoka United mwishoni mwa dirisha hili la usajili na ametoa upadate nyingine kwa mashabiki wake

Kupitia ukurasa wake wa Twitter ametweet hivi: “Baada ya mizunguko yangu, nafurahia muda uliosalia katika siku ya leo hapa Manchester. Natumaini wote mna siku njema!”
United wanaonekana hawana mpango tena na Schweinsteiger na kaka yake Bastian, Tobi Schweinsteiger alinukuliwa akikosoa kitendo hicho alichofanyiwa mdogo wake na ku-tweet: “No respect.”
Mpaka sasa, United wanaviungo wa kati watano ambao ni Paul Pogba, Michael Carrick, Morgan Schneiderlin, Marouane Fellaini na Ander Herrera.
Ripoti zinaeleza kwamba, klabu za AC na Inter Milan zinahitaji huduma ya Schweinsteiger, ambaye atatakiwa kupunguza sana mshahara wake endapo ataamua kuondoka.
Anatajwa kupokea kiasi cha paundi 200,000 kwa wiki.
Msimu uliopita, Schweinsteiger alianza kwenye michezo 21 na michezo 10 aliingia kutokea benchi.

Hizi ndio Sababu kwanini Paul Pogba amefungiwa kucheza vs Bournemouth

Kiungo mpya wa Manchester United Paul Pogba amesimamishwa kuitumikia timu yake kwa mchezo wa kwanza wa Premier League,  chama cha soka cha England kimethibitisha. 
Pogba, 23, alirejea Old Trafford kutoka Juventus kwa ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya £89.3 million, miaka 4 baada ya kuhamia klabu ya Turin kwa ada ya £800,000 kufuatia kukosa muda wa kucheza na mgogoro wa mkataba mpya. 
Hata hivyo Pogba itambidi asubiri mpaka wiki ijayo kucheza mchezo wake wa kwanza na klabu yake mpya kwa sababu amefungiwa kucheza mchezo wa Jumapili dhidi ya Bournemouth. 

Kiungo huyo wa Ufaransa amesimamishwa kwa kosa la kupata kadi mbili za njano katika msimu uliopita wa mashindano ya Coppa Italia, na adhabu yake imehamia katika michezo inayosimamiwa na Chama cha soka cha England.

Maamuzi ya Juan Mata baada ya kuhisi maisha Old Trafford yatakuwa magumu kwake

Kitendo cha kocha mpya wa Man United Jose Mourinho kumuingiza Juan Mata dakika ya 63 na kumtoa katika dakika za nyongeza katika mchezo wa ngao ya hisani dhidi ya Leicester City, kinaonekana kuchukuliwa tofauti na kutabiriwa kuwa maisha ya nyota huyo Old Trafford yatakuwa magumu.

Stori kutoka The Times inaripoti kuwa Juan Mata kwa sasa analazimisha klabu imuachie aondoke licha ya kuwa uongozi wa Man United hawana mpango wa kumuuza kwa sasa, lakini gazeti hilo pia linaripoti kuwa kocha wa Everton Ronald Koeman kaonesha dhamira ya kumuhitaji staa huyo.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri suala la Juan Mata kuhusishwa kuondoka linatarajiwa kutokea kutokana na Jose Mourinho kudaiwa kutomuhitaji, hali kama hiyo iliwahi kumkuta Juan Mata wakati yupo Chelsea na Jose Mourinho ila mwaka 2014 aliamua kuondoka klabu hiyo na kujiunga na Man United.

Friday, May 6, 2016

we are back in accumulator tips


Sligo Rovers vs Wexford Youths
#pick Sligo Rovers AH -1.0
#odds 2.05

AH means Asian Handcap

Friday, February 19, 2016

acculator tips 20/02/2016

Arsenal v Hull
#odds 1.50

Mansfield v Dagenham and Redbridge
#odds 1.80

Forest Green v Eastleigh
#odds 1.95

Harrogate Town v  United of manchester
#odds 1.60

Le Havre v Creteil
#odds 1.50

AZ v FC Groningen
#odds 1.51

Pacos Ferreira v Benfica
#odds 1.30

PSV v Heracles
odds ?

Lokeren v Genk
#odds 2.20

Winterthur v Schaffhausen
#odds 1.90

Asteras Tripoli v PAS Giannina
#odds 1.61

Ferencvarosi v Puskas
#odds 1.30

Dinamo Bucharest v CS Concordia Chiajna
#odds 1.70


mkeka wa handicap weekend hii (betting tips 20/02/2016)

Burnley v Rotherham
#pick burnley  Asian Handicap  -1.0
# odds 1.98

Cagliari v Pescara
#pick Cagiliar Asian Handcap -1.0
# odds 2.30

Pacos Ferreira v Benfica
#pick Benfica Asian Handcap 1.5
#odds 1.98


Sunday, February 14, 2016

Arsenal vs Leicester City 2-1 All Goals & Highlights 2016


VIDEO::HIGHLIGHT ZA MECHI ZOTE ZA EPL JANA FEB 13


Chelsea v Newcastle 5-1 Norwich v WestHam 2-2 WBA v Everton 1-0 Sunderland v Manchester United 2-1 Bournemouth vs Stoke City 1-3

Video ya magoli yote ya mechi ya Stand United Vs Simba Feb 13 2016, Full Time 1-2

Klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba February 13 2016 ilishuka dimbani kuvaana na wenyeji wao klabu ya Stand United katika mchezo wake wa 19 wa Ligi Kuu Tanzania bara, Simba walifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1, magoli ya Simba yalifungwa na Hamis Kiiza dakika ya 37 na 47, wakati goli la kufutia machozi la Stand United lilifungwa dakika ya 89 na Pastore Atanus. Hii ni video ya magoli yote mtu wangu yaliofungwa katika mechi hiyo.

Post Labels