Akizungumza
na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa
Polisi wa kanda hiyo, Hezron Gymbi amesema watuhumiwa hao walikamatwa
jana maeneo ya Chamanzi muda mfupi baada ya kukutana na kupanga kufanya
uhalifu wa kutumia silaha.
Watuhumiwa
hao wanaofahamika kwa majina ya Uswege Seleman (23), Hassan Abdallah
(73), Said Kiwambu (39) na Hamadi Badrilu (28) walikutwa na silaha aina
ya MARK 4 yenye namba LA-227725A baada ya askari polisi kufanya upekuzi
katika nyumba waliyokutana.
Kukamatwa
kwa watuhumiwa hao kumefuatia baada ya raia mwema kutoa taarifa kwamba
kuna watu wanaoshukiwa kuwa majambazi wanaotumia silaha katika matukio
mbalimbali kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Tanga na
Lindi.
Post a Comment Blogger Facebook