Watanzania
wanne wamethibitishwa kufa katika tukio la kukanyagana jana huko Mina
katika mji wa Mecca, ikiwa ni miongoni mwa mahujaji 717 waliopoteza
maisha katika tukio hilo wakati wa siku ya mwisho ya Hija.
Taarifa
ya Sheikh Mkuu wa Tanzania Mufti Abu Bakari Zuberi iliyotolewa akiwa
Mecca imewataja watanzania watatu waliokwisha tambulika majina yao kuwa
ni Bi. Mwanaisha Hassan Juma, Mkungwe Suleiman Hemedi na Sefu Saidi
Kitimla.
Mtanzania
mwingine mwanamke aliyekufa jina lake bado halijatambulika, pia yupo
raia mmoja wa Kenya Bi. Fatuma Mohammed Jama ambaye alisafiri Mecca kwa
kutumia wakala wa Tanzania.
Post a Comment Blogger Facebook