ZOTEHAPA BLOG

Wednesday, February 3, 2016

Gari la CRDB laopolewa, mfanyakazi hajapatikana


 Gari hilo liliopolewa jana saa nane mchana baada ya kulitafuta kwa siku tano tangu lilipozama Mto Kilombero Januari 27 likiwa katika kivuko cha MV Kilombero II.
Kilombero. Gari la Benki ya CRDB limeopolewa katika Mto Kilombero likiwa na Sh3.5 milioni, huku mfanyakazi wake akiwa hajapatikana.

Gari hilo liliopolewa jana saa nane mchana baada ya kulitafuta kwa siku tano tangu lilipozama Mto Kilombero Januari 27 likiwa katika kivuko cha MV Kilombero II.

Mfanyakazi wa CRDB tawi la Ifakara, Dustan Rwegasira (31) ni miongoni mwa abiria waliokuwamo ndani ya kivuko hicho.

Hata hivyo, jitihada mbalimbali za kukiibua kivuko hicho bado zinaendelea baada ya juzi kutumia mbinu ya kutumbukiza mapipa yaliyojazwa maji kisha kuzamishwa chini ili kukitoa kukwama.

Kazi hiyo inafanywa na timu ya wazamiaji wa Kampuni za M.Divers Limited na May-Marine Go Limited.

Mkuu wa Kikosi cha Uzamiaji na Uokoaji wa Kampuni ya M. Divers Limited, Hafidh Seif alisema: “Hesabu zetu zinakwenda vizuri, yale matangi unayoyaona yanazamishwa baada ya kujazwa maji halafu, yakiwa chini yatageuka maboya kisha yatapanda juu na kivuko hicho na kuvutwa na wenye magari,” alisema Seif.

Seif alisema wanakabiliana na changamoto ya kasi ya maji, lakini wanamshukuru Mungu kazi ya kuondoa maji ndani ya vyumba vya maboya ya kivuko imemalizika salama. 


Posted by Unknown at 4:55:00 AM
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Labels: KITAIFA

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Post Labels

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();
.disqus.com/recent_comments_widget.js?num_items=4&avatar_size=32&excerpt_length=100&hide_mods=0">

Labels

Breaking News

Main Menu

Top Menu

Contact us

Name

Email *

Message *

twitter

Tweets by @zotehapa1

facebook

Zotehapa1

mapenzi na simulizi

Popular Posts

  • Mahabusu Ajinyonga Arusha
    Mahabusu aliyekuwa akishikiliwa katika kituo kikuu cha polisi jijini Arusha aliyetambulika kwa jina la Victoria Wenga (51) mkazi wa ...
  • AliKiba akanusha kuwepo kwenye show ya Uganda Entertainment Awards
    Mkali wa wimbo ‘Aje’ AliKiba amekanusha taarifa zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kuwa atafanya show katika utowaji wa tuzo za Ugan...
  • Usharobaro Wamtokea Puani Stan Bakora
    Usharobaro umemtokea puani komediani wa Bongo, Stanley Yusuph ‘Stan Bakora’ baada ya kudondoka na kuumia mguu wa kulia wakati akifanya ma...
  • DI MARIA KATUA RASMI PSG
    Klabu ya Paris Saint German ya ufaransa imefanikiwa kupata sahihi ya aliyekuwa mcheza wa Manchester United ya Uingereza Angel Dimaria Na a...
  • CHOMBEZO: KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA....SEHEMU YA.... 01
    CHOMBEZO: KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA....SEHEMU YA.... 01 Mtunzi_Na: IRENE MWAMFUPE NDAUKA “Mke wangu, kilasiku namwona huyu kijana m...
  • MAGUFULIA AKIWA MBEYA AKIENDELEA NA KAMPENI
     Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuliakihutubia wakazi wa Mbalizi na kuendelea kusisitiza elimu itakuwa bure kuanzia da...
  • Baadhi ya wajumbe ZEC hawaungi mkono uchaguzi wa marudio Zanzibar.
    Baadhi ya wajumbe wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC ambao hawaungi mkono uchaguzi wa marudio wamemtaka mwenyekiti wa tume hiyo Jecha Sa...
  • WATCH FEZA KESSY FT CHEGE - SANUKA - OFFICIAL VIDEO
    feza kessy
  • Ukawa Sasa Kutoa Msimamo Wao Juu ya Suala la Zanzibar
    Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akihojiwa na wanahabari (picha na maktaba). UMOJA wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) um...
  • Olimpiki: Mwanariadha wa Kenya Apokonywa Medali Kwa Kosa la Udanganyifu
    Mwanariadha kutoka nchini Kenya aliyeshinda medali ya shaba kwenye riadha na kuruka vihunzi pamoja na maji, Ezekiel Kemboi amepokonywa ...

About us

ads

youtube

ads

UDAKU

Awesome Inc. theme. Powered by Blogger.