0
Msanii mkongwe wa Hip hop nchini Afande Sele amefunguka na kumuombea mabaya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi na kusema ni bora aende kwani katika kipindi chake hakuna jambo lolote la maendeleo amelifanya.

Afande Sele ametumia ukurasa wake wa facebook na kusema yake ya moyoni kwa kulinganisha ofisi na hatua ambazo zimepigwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Sudan na kusema Malinzi anapaswa kuondoka tu kwani ni aibu.

"Ofisi ya chama cha soka cha Sudan na ofisi ya chama cha soka Tanzania..aibu yetu..acha Magufuli atunyooshe tu kwani tulizidisha uwendawazimu. Nenda Malinzi nenda tuuu" alisisitiza Afande Sele

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi ambaye alikuwa ni mmoja kati ya watu ambao walikuwa wanagombea nafasi ya Urais katika shirikisho hilo lakini jina lake lilienguliwa katika mchakato huo baada ya kushindwa kuhudhuria katika usaili wa wagombea uliofanyika siku ambayo yeye yupo rumande kutokana na kesi inayomkabili ya matumizi mabaya ya ofisi.

Post a Comment Blogger

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();
 
Top